Na Shushu Joel
SHEIKH mkuu wa Baraza kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Muft Abubakar Zuberi amemthibitisha Alhaj Sharifu Zahoro kuwa Barozi wa dini ya kiislamu.
Mufti Abubakar Zuberi akifafanua jambo mbele ya waumini wa dini ya kiislamu juu ya umuhimu wa kusoma
Akizungumza na umati wa viongozi, waumini na wanafunzi wa
dini ya kiislam katika hafla ya kuhitimu kwa wanafunzi wa Bakwata online
Academy (TEHAMA) Muft Zuberi alisema
kuwa kazi ya ubalozi ni kubwa na yenye heshima kubwa katika dini yetu hivyo
tumemkabidhi kazi hiyo Sharifu kutokana na utendaji wake wa kazi mbalimbali za
kijamii.
“Awali nilitaka awe Balozi wa Mkoa wa Pwani lakini kutokana
na utendaji wake kazi mbalimbali na tabia njema aliyonayo nimeamua awe balozi
wan chi nzima kwani atakuwa msaada mkubwa katika Taifa letu”Alisema Muft Zuberi
Aidha alisema kuwa waislamu kila kikicha tunarudi nyuma kutokana na sababu za baadhi ya watu kuwa na tabia za wivu,ubinafsi, na ndio maana tumekuwa tukichelewa sana katika kufanya maendeleo mbalimbali kwa kusudi la kulisaidia Taifa letu.
Baadhi ya viongozi mbalimbali wa dini ya kiislam wakimpongeza Balozi Sharifu mara baada ya kuthibitishwa kuwa balozi na Muft Abubakar Zuberi
Kwa upande wake Balozi Sharifu Zahoro mara maana ya
kuthibitihwa na Mufti Zuberi alisema kuwa kazi ya Mungu ni kujitolea hivyo
nitahakikisha najitolea kwa moyo wangu wote ili tufike kule tunapopahitaji
kufika.
Pia Balozi Sharifu amewasisitiza waumini wote wa dini ya
kiislam na watanzania kwa ujumla kuendelea kutoa ushirikiano kwake kwake bila
wao hawezi kufanya kitu chochote chenye tija.
MWISHO
0 Comments