MWENYEKITI WA WAZAZI AWAKUMBUSHA WAZAZI KUWAKANYA WATOTO

Na Shushu Joel,Bagamoyo.

MWENYEKITI wa jumuiya ya wazazi(CCM)  Mkoa wa Pwani Jackson Kituka amewataka wazazi wote wilaya ya Bagamoyo kusimamia maadili mema kwa watoto wao kama ilivyokuwa miaka ya zamani kwa upande wao walivyosimamiwa na wazazi hao.

Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi Mkoa wa Pwani Jackson Kituka akisisitiza jambo mbele ya viongozi wa kata hawapo pichani(NA SHUSHU JOEL)

Rai hiyo ameitoa alipokuwa akizungumza na viongozi wa jumuiya hiyo wilaya ya Bagamoyo kwenye kikao maalum alichokifanya Mwenyekiti huyo ambacho kilikuwa na lengo la kuimalisha jumuiya hiyo .

Aliongeza kuwa watoto wetu wamekosa maadili mema tuliyofanikiwa kuyapata sie kipindi cha nyuma hivyo kama wazazi ni lazima tukumbushane umuhimu wa kuwasimamia watoto wetu ambao wameshindwa kuwa na maadili mema huku taifa likiwategemea kwenye masuala mbalimbali.

“Sie tumebahatika kulelewa kwenye misingi ya kuwa na adabu na maadili ya hali ya juu lakini nashangazwa na kizazi cha sasa kuporomoka kwenye maadili huku watoto hao wakitokea kwenye majumba yetu”Alisema Mwenyekiti wa wazazi Mkoa huo wa Pwani Ndg Kituka.

Baadhi ya wajumbe wakimsikiliza Mwenyekiti wa wazazi Ndg Jackson Kituka 

Kwa upande wake Shabani Juma(67) mmoja wa wazazi waliohudhulia kikao hicho amempongeza Mwenyekiti huyo kwa kutambua na kuona ni jinsi gani watoto wetu walivyoporomoka kimaadili.

Aidha amemwakikishia Mwenyekiti huyo kuwa kupitia nafasi yake ya uongozi ndani ya jumuiya hiyo atahakikisha anatumua muda mwingi kuwakumbusha wazazi wengine kuhakikisha wanawasimamia watoto kwenye misingi iliyo imara.

Naye Bi,Khadija Ally amempongeza Mwenyekiti huyo kwa maono yake ya mbali juu ya kuporomoka kwa maadili ya vijana wetu.

Pia amewakumbusha wazazi kuwa na tabia ya kufuatilia mienendo ya watoto wetu kama ilivyokuwa kipindi chetu ambacho wazazi wetu walikuwa wakitufuatilia kwa kila hatua ambayo tulikuwa tukiipiga na ndio maana leo hii wengi wetu tumekuwa wazazi wa mifano hivyo ni lazima kila mzazi awe makini na watoto wake na wa mwenzake kwa kusudi la kurudisha maadili kwa vijana wetu

MWISHO

Post a Comment

0 Comments