BUKOMBE YAFUNGUA MILANGO YA KUJIFUNZA NAMNA YA UTEKELEZAJI MIRADI.

Na Shushu Joel

Moja ya majengo ya shule yaliyojengwa na halmashauri ya Bukombe chini ya usimamizi wa Mkurugenzi Mtendaji George Lutengano(NA SHUSHU JOEL)

MKURUGENZI mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Bukombe Mkoani Geita George Lutengano amefungua milango kwa watu mbalimbali kuweza  kwenda katika halmashauri hiyo na kuwenza kujifunza namna jinsi wanavyofanikiwa kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kiwango cha hali ya juu.

Akizungumza na waandishi wa habari Lutengano alisema kuwa Bukombe imekuwa ikitumia pesa zote zinazoletwa na serikali  kwa ajili ya maendeleo ya wananchi kwa kufanya kile kilichokusudiwa kufanyika kwa wananchi.

“Bukombe imetekeleza miradi mbalimbali ambayo ilikuwa ni sugu na hata mingine mingi mipya kwa kusudi la kuondoa changamoto kwa wananchi wetu ambao kipindi hiki cha Rais Samia Suluhu Hassan wamekuwa na neema kubwa ya uwepo wa miradi mingi” Alisema Lutengano.

Pia alisema kuwa halmashauri ya Bukombe imefanikiwa kukamilisha miradi mbalimbali ikiwemo shule za msingi na sekondari,miradi ya Afya,Nyumba za watumishi,Maji na miundombinu vyote vikiwa ni utekelezaji wa wa serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan

Naye Paul Fumbuka mkazi wa Ushiromba amempongeza Mkurugenzi mteandaji wa halmashauri ya Bukombe kwa jinsi ambavyo amekuwa mbunifu wa kuongeza mapato ya halmashauri na vile ambavyo amekuwa akitekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwa ajili ya wananchi wa halmashauri ya Bukombe.

“Sisi wananchi wa Bukombe tunamshukuru sana Mhe: Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea mkurugenzi mwenye uchu wa maendeleo kwa kuwaona wananchi wanakuwa karibu na miradi muhimu kama vile Afya, miundombinu na miradi ya elimu” Alisema Fumbuka.

Mwisho

 

 

 

Post a Comment

0 Comments