Na Shushu Joel
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewakosha wananchi wa wilaya ya Bukombe Mkoani Geita kwa kuwashushia neema ya miradi mingi ya maendeleo kwenye maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.
![]() |
Mkuu wa wilaya ya Bukombe Said Nkumba |
Akizungumza
na waandishi wa habari Mkuu wa wilaya ya Bukombe Said Nkumba alisema kuwa Serikali
ya awamu ya sita chini ya Rais Mama Samia Suluhu Hassan imekuwa msaada mkubwa
kwa wananchi wa Bukombe kutokana na fedha nyingi za utekelezaji wa miradi.
“Bukombe
tunamshukuru sana Rais Samia kwa utendaji wake wa kazi kwa kutushushia fedha za
miradi kwa jamii na kutekeleja miradi yenye uhitaji mkubwa kwa wananchi”Alisema
Nkumba
Aidha
alisema kuwa wilaya ya Bukombe umepata fedha nyingi na imefanikiwa kutekeleza ujenzi wa miradi kwa kiwango cha
hali ya juu kutokana na usimamizi mzuri wa viongozi wa wilaya hiyo.
Aliongeza
kuwa miradi iliyotekelezwa ni ujenzi wa shule,Nyumba za watumishi wa idara
mbalimbali, Huduma za maji, Barabara na Taa za kisasa za barabarani kitu
ambacho kinapelekea wilaya yetu kukosekana kwa usiku wala mchana kwani muda
wote mji wetu unapendeza.
Kwa upande
wake Bi, Maria Sololo (76) Mkazi wa Lunzewe alisema kuwa kwa kweli kipindi cha
Rais Samia Suluhu Hassan maendeleo mengi yanafanyika ikilinganishwa na vipindi
vingine hii ni kutokana na uchungu wa maendeleo alio nao Rais wetu Mhe. Samia
kwa wananchi wake.
Aliongeza kuwa nimewaona marais wengi lakini Mhe. Samia amekuwa mkombozi mkubwa na hasa kwetu kina Mama kwani jinsi ambavyo hataki kutuona tukiangaika na masuala ya maendeleo ambayo yapo ndani ya uwezo wake.
“Awali
tulikuwa hatujua ni kwnini Rais wetu anakwenda nje ya nchi kumbe ni
kutuangaikia wananchi wake hivyo mimi namuombea Rais Samia apambane anavyojua
ili wananchi wake tuneemeke kama anavyofanya sasa kwenye miradi
mbalimbali”Alisema Bi, Maria
Aidha
alisema kuwa kwa wilaya yetu ya Bukombe ni mengi yamefanyika chini ya Rais
kipenzi Mhe.Samia Suluhu Hassan.
MWISHO
0 Comments