“YAJAYO BUKOMBE YANAFURAHISHA”DC NKUMBA

Na Shushu Joel, Bugombe.

MKUU wa wilaya ya bukombe Mkoani Geita Said Nkumba amewaeleza wananchi wa wilaya hiyo kuwa wilaya yetu itaendelea kupata miradi mingi na yenye uhitaji kutokana nan a malengo ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Shupavu Mhe: Samia Suluhu Hassan.

Mkuu wa wilaya ya Bukombe Said Nkumba akizungumza na waandishi wa habari nofisini kwake.
9NA SHUSHU JOEL)

Akizungumza ofisini kwake na waandishi wa habari Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa Rais Samia Suluhu Hassan ni msikivu na ni mpenda maendeleo kwa watu wake hivyo wana Bukombe tuendelee kumuombea Rais wetu ili aweze kufaniklisha ndoto zake za kuiona Tanzania ikiwa kwenye mabadiliko ya hali ya juu katika sekta mbalimbali za kimaendeleo.

Aidha alisema kuwa mpaka sasa wilaya yetu ya Bukombe imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kitu ambacho hapo awali ilikuwa ni changamoto kwa wananchi.

“Tuendelee kumuombea Rais wetu ili aweze kuwa na Afya njema ili azidi kututumikia wananchi wake wa Bukombe”Alisema Nkumba

Mpaka sasa Rais Samia Suluhu Hassan kafanikisha uwepo wa  miradi mingi na yenye gharama kubwa  katika wilaya yetu ikiwemo Vituo vya Afya,shule za msingi na sekondari katika maeneo ambayo yalikuwa hayana shule kabisa na zingine zilikuwa shule shikizi,huduma za upatikanaji wa maji ya uhakika katika baadhi ya maeneo ya wilaya yetu,miundombinu ya barabara kupitia wakala wa barabra vijijini na zile za Tanroad hivyo uwepo wa vitu hivi vimepelekea kupatikana kwa maendeleo ya haraka kwa wananchi wa Bukombe.

Juma Milanzi ni mkazi wa Bukombe anasema kuwa kilichofanyika Bukombe kupitia Rais Samia Suluhu Hassan ni hatua kubwa sana kwani ilikuwa tukiviona sehemu za mijini tu lakini kwa sasa nasi tunavyo.

 

Aliongeza kuwa Bukombe sasa tuna taa za barabarani kitu ambacho kimechangia kutokomeza changamoto nyingi ikiwemo wizi na kuongeza thamani ya wilaya yetu ya Bukombe.

“Niwaombe nwananchi wenzangu wa Bukombe kuendelea kumuombea Rais wetu Samia Suluhu Hassan ili azidi kuiona Bukombe yetu katika maendeleo” Alisema

MWISHO

Post a Comment

0 Comments