SERIKALI YAELEKEZA KIWANDA KUTATUA CHANGAMOTO YA KIMAZINGIRA

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis
Hamza Khamis akitoa maelekezo wakati wa ziara ya kikazi ya katika kiwanda



 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis

Hamza Khamis ameelekeza kiwanda cha nguo cha A to Z kilichpo mkoani Arusha

kikamilishe ujenzi wa mtambo wa kutibu majitaka ndani ya miezi miwili.

Ametoa maelekezo hayo jana alipofanya ziara ya kukagua na kufuatilia

utekelezaji wa maagizo ya Serikali kuhusu kuondoa changamoto ya harufu na

majitaka yanayotirirka kupita mtaro unaopita kwenye makazi ya watu.

Pia, ameelekeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)

Kanda ya Kaskazini, wataalamu wa mazingira kutoka Ofisi za Mkuu wa Mkoa,

Wilaya na Halmashauri ya jiji la Arusha kufanya kazi kwa pamoja kuhakikisha

maeleekzo hayo yanatekelezwa.

“Hamuwezi kujua hizi harufu mbaya za haya majitaka yanayotoka hapa na

kutiririka kwenye makazi ya watu zina athari gani, sasa ninatoa miezi miwili

mkamilishe mtambo wa huu,” alisema Mhe. Khamis.

Aidha, naibu waziri huyo alisema kiwanda hicho kimekuwa kikilamikiwa na

wanachi kwa muda mrefu kwa uchafuzi wa mazingira kwa kutiririsha majitaka

katika makazi ya wananchi.


Hivyo, kutokana na hali hiyo Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kwa

kutoa maeleekzo kwa uongozi wa kiwanda kujenga mtambo wa kusafishia

majitaka kabla ya kwenda kwenye mazingira.

Akikagua ujenzi wa mtambo huo Naibu Waziri ameridhika na utekelezaji wa

mradi huo na kuwataka uongozi wa kiwanda hicho kukamilisha mara moja

mtambo huo.

Alisema Serikali inawapenda wawekezaji lakini wakati huohuo inalinda afya za

wananchi wake pamoja hifadhi ya mazingira lakini kiwanda hicho kimekuwa

kikilamikiwa na wananchi kuhusu kuchafua mazingira.

Awali Meneja wa NEMC Kanda ya Kaskazini Bw. Lewis Nzali alisema baraza hilo

limekuwa likitoa maelekezo mbalimbali ikiwemo kukipiga kiwanda hicho faini kwa

uharibifu wa mazingira.

Meneja huyo alisema kuwa kutokana na hatua hizo kiwanda cha A to Z kimeweza

kuanza kujenga mtambo wa kuchakata majitaka kabla ya kwenda kwenye

mazingira.


Nzali aliongeza kwa kusema kuwa hata hivyo hatua hiyo imeleta mafanikio katika

sekta ya uwekezaji nchini kwa kuweza kuzingatia Sheria ya Mazingira ya Mwaka

2004.

Kwa upande wake Meneja wa Kiwanda cha A to Z Bw.Sylivester Kazi aliahidi

kukamilika kwa ujenzi wa mtambo huo ili kulinda afya za wananchi

wanaozunguka eneo hilo.

Mtambo huo umegharimu kiasi cha sh. Bilioni 1 ambapo kukamilika kwake

kutaondoa tatizo la majitaka kutiririka katika makazi ya wanachi na kusambaa

kwa harufu mbaya.

Alisema baada ya kukamilika kwa mtambo huo majitaka yote yataunganishwa na

mradi wa kuondosha majitaka wa Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Arusha

(AUWSA) hayatapita tena katika mtaro huo unaotumika sasa.

Post a Comment

0 Comments