SABABU ZINAZOFANYA RC KUNENGE KUFANIKIWA PWANI

Na Shushu Joel,Pwani

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge  amezidi kuwa kinara katika ufanikishaji wa kila jambo ambalo amekuwa akiliofanya kwa jamii ya wakazi wa mkoa huo, kitu ambacho kimepelekea kuupaisha Mkoa huo katika Nyanja mbalimbali za kimaendeleo.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge akisistiza jambo .(NA SHUSHU JOEL)

Kusudi la Mkuu huyo wa Mkoa wa Pwani katika ufanisi mkubwa wa kubuni mambo mengi yanayojkenga maendeleo ni kuwakutanisha wananchi na wazalishaji yaani wamiliki wa viwanda na wakulima wa chini kabisa ambao wamekuwa wakililia upatikanaji wa masoka ya kile wanachokizalisha,

Timu ya Blog ya  HABARI MPYA MEDIA imefanya utafiti mdogo  kwa jamii ili kujua ni sababu ipi inayopelekea kila jambo linalosimamiwa na Mkuu huyo wa Mkoa wa Pwani Kunenge limekuwa likifanikiwa kwa asilimia kubwa na kufanikiwa kupata baadhi ya maoni ya wananchi mbalimbali juu ya suala la ufanisi unaofanywa na Kunenge.

Juma Hassan ni mkazi wa Matipwili kata ya Mkange katika halmashauri ya Chalinze mara baada ya kufanya mahojiano na mwandishi wa Makala hii alisema kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Kunenge amekuwa akifanikiwa kutokana na kuwashirikisha jamii ya watu wa chini na kuwauliza nini hitaji lao ambalo uenda lilikuwa sugu au la sasa na wanataka lifanikiwaje hivyo katika mambo hayo Mkuu wetu wa Mkoa amekuwa akifanikiwa sana.

Pia jambo lingine ambalo limekuwa likimbeba Kunenge ni kubadikisha changamoto kuwa fursa na hivyo baadhi ya wananchi wa hali ya chini kuzidi kunufaika na kile kilichopo ndani ya Mkoa wao.

Aidha tumuombe Mkuu wetu wa Mkoa azidi kutafuta wawekezaji wa viwanda kwani wamezidi kuwa wakombozi wa suluhisho wa mambo mbalimbali ikiwemo ajira, uuzaji wa mali ghafi kwa jamii zinzokuwa zimezunguka eneo hilo.

Kwa upande wake Bi. Fatma Haji (65) mkazi wa kata ya Nia Njema wilaya ya Bagamoyo mara baada ya kufanya mazungumzo na HABARI MPYA MEDIA  alisema kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani amekuwa akifanikiwa vitu vingi kutokana na juhudi zake binafi anazowafanyia wananchi wa Mkoa huo na hasa  katika kusukuma maendeleo.

“kwa kweli tumefanikiwa kupata Mkuu wa Mkoa mwenye uchu mkubwa wa maendeleo tunaamini Pwani tutafika mbali katika maendeleo”Alisema Bi, Fatma.

 

Aidha amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mamama Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo akiiangalia Pwani kwa jichio kubwa katika ufanisi wa miradi ya maendeleo.

MWISHO

 

 

Post a Comment

0 Comments