BIBI TITI AZIDI KUENZIWA KWA USHUJAA WAKE

Na Shushu Joel, Rufiji

ALIYEKUWA Mwenyekiti wa kwanza wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania Hayati Bibi Titi Mohamed amezidi kukumbukwa na jumiya hiyo kwa kuenzi yale aliyokuwa akiyafanya kwa vitendo.

Wanawake katika Mkoa wa Pwani wamekutana katika wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani kwa kusudi la kuonyesha mapenzi yay a dhati kwa kuyafanya yale ambayo Bibi Titi alikuwa akiyafanya kwa jamii yote ya watanzania.

Aidha aliongeza kuwa Wanawake tukiwa wamoja basi mambo mengi yatafanikiwa na hasa miradi mbalimbali.


“Nimpongeze Rais Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo amekuwa nguzo ya Taifa hili kwa jinsi ambavyo amekuwa akishusha maendeleo kwa watanzania.

Akizungumza mara baada ya kikao kazi Mjumbe wa mkutano Mkuu wa Jumuiya hiyo na ambay pia ni mbaraza Mariam Ulega alisema kuwa ni jambo la faraja kwetu Wanawake Mkoa wa Pwani kwa kufanya maadhimisho ya kumbukumbu hayo katika Mkoa wetu.

Alisema kuwa Bibi Titi amefanya mambo mengi katika Taifa hili ndio maana amekuwa akienziwa kwa wema wake.

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo katika Mkoa wa Pwani Zaynabu Vulu amewasifia Wanawake kwa jinsi ambavyo wamejitokeza katika maadhimisho hayo.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments