VULU ATAKA BIBI TITI MOHAMED AANZISHIWE TAASISI.

 Na Shushu Joel, Rufiji. 

MWENYEKITI wa Jumiya ya Umoja wa Wanawake  Tanzania Mkoa wa Pwani Bi  Zaynabu Vulu ameitaka Wizara ya Sanaa,Michezo na Utamaduni kuweza kuanzisha Taasisi ya kumbukumbu ya Bibi Titi Mohamed kama ilivyo kwa taasisi zingine za wasisi wa Taifa letu kama vule taasisi ya  Mwalimu Nyerere.

Aliongeza kuwa endapo tukianzisha taasisi hiyo itakuwa ni msaada mkubwa kwa kizazi cha sasa na kijacho kuweza kumtambua kwa ufasaha Hayati Bibi Titi Mohamed alikuwa ni kiongozi wa namna gani katika Taifa lake 


Aidha alisema kuwa ni vyema sasa maadhimisho ya kumbukumbu ya Bibi Titi Mohamed yakafanyika katika Mikoa mbalimbali kwa kusudi la kuijua historia yake ya Hayati Bibi Titi.


Kwa upande wake Mariam Ulega ambaye ni mbaraza kutokea Mkoa wa Pwani amewapongeza wote walioshiriki katika maadhimisho hayo ya kumuenzi Hayati Bibi Titi Mohamed pia wamejua historia ya mwasisi huyo wa  UWT Taifa.


Aidha amewataka wanawake wote nchini kufuata  mienendo  ya Hayati Bibi Titi Mohamed. kama alivyokuwa akiitendea haki jumuiya hiyo.


MWISHO

Post a Comment

0 Comments