SERIKALI YAMEGA MAENEO YA RANCHI YA KAGOMA NA KUYAGAWA KWA WANANCHI MULEBA

 Na Shushu Joel

Serikali imemega baadhi ya maeneo ya Ranchi ya Kagoma yenye ukubwa wa

hekta 50,690 na kuyarasimisha kwa wananchi wa Kata ya Rutoro wilayani

Muleba mkoani Kagera ili kwa ajili ya shughuli za makazi, kilimo na ufugaji .

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb)  akiwahimiza wananchi kuanzisha miradi ya upandaji miti na ufugaji nyuki katika maeneo watakayokabidhiwa na Serikali wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la Shule ya Msingi Rutoro, Wilayani Muleba Mkoani Kagera.

Kauli hiyo imetolewa  na Kamati ya Mawaziri wa Kisekta katika mkutano

wa hadhara uliofanyika katika eneo la Shule ya Msingi Rutoro, Muleba .


 Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (Mb) amesema maeneo

hayo yatamegwa na kupewa wananchi kwa kuzingatia ushauri wa watalaam.


“Maeneo yatakayomegwa kwa kuzingatia ushauri wa wataalamu kutoka

kwenye ranchi yatawekewa utaratibu wa usimamizi na uongozi wa mkoa

ukishirikiana na wilaya ili msigombanie au kufanya jambo lolote ndani ya

maeneo hayo” Mhe. Ndaki amesisitiza.



Mhe. Ndaki amewaonya viongozi wa vijiji na vitongoji kuacha tabia ya kugawa

maeneo hayo kwa kuwa hawana mamlaka ya kugawa maeneo.


Katika hatua nyingine, amesema Serikali imeridhia kukiacha Kitongoji cha

Rwamisha B ambacho kiko wilaya ya Karagwe chenye kaya 480 ambacho

awali kiliamuliwa kiondoke.


Mhe. Ndaki ameelekeza mkoa wa Kagera kuandaa mpango wa utekelezaji

wa maamuzi ya Kamati ya Mawaziri ya Kisekta yaliyofikiwa ikiwa ni pamoja

na kurekebisha mipaka ya vijiji kwa kuzingatia maoni ya wataalamu.


Sambamba na hilo Waziri Ndaki amewatoa hofu wawekezaji walioko katika

Ranchi ya Kagoma akiwaeleza kuwa wako salama na Serikali imefanya

mazungumzo na Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) ili uwekwe utaratibu

mzuri ambao utawawezesha kupewa maeneo yatakayomegwa.


Amewaasa wananchi kuwa watulivu wakati wa utekelezaji wa maamuzi ya

kamati hiyo na kuacha kuvamia maeneo ili kurahisisha utekelezaji wa

maamuzi hayo.



Naye, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.

Ridhiwani Kikwete (Mb) amewataka wananchi kuendelea kuheshimu sheria

za ardhi hususani katika mpango wa maendeleo ya ardhi na kwamba kuna

kazi ya kufanya katika kuhakikisha miundombinu na majengo ya eneo la

Rutoro yanakaa sawa.


Ametoa rai wananchi hao kuwa watulivu mpaka wataalamu wa ardhi

watakapokuja kutoa utaratibu wa maeneo yaliyoachiwa kwa wananchi.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja

(Mb) amewataka wananchi wa Kata ya Rutoro kuitumia ardhi waliyoachiwa

kwa maendeleo kwa kuanzisha miradi ya upandaji miti pamoja na ufugaji

nyuki.


“Nendeni mkapande miti kibiashara mtapata mbao na wakati huohuo

mnaweza kuanzisha miradi ya ufugaji nyuki.


Ametoa wito kwa wananchi kutoyavamia maeneo yatakayoachwa kwa

Serikali kwa kuwa ni maeneo yanayotunzwa kwa faida ya kizazi cha leo na

kinachokuja.


Kamati ya Mawaziri wa Kisekta imehitimisha ziara yake mkoani Kagera na

itaendelea na zoezi hilo katika mkoa wa Ruvuma.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments