“RAIS DKT SAMIA CHANZO CHA HAPA TULIPO” MARIAM ULEGA

Na Shushu Joel,Mkuranga

MJUMBE wa Baraza Kuu  wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kutokea Mkoa wa Pwani Bi’ Mariam Ulega amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo amekuwa msaada mkubwa kwa wananchi kutokana na jinsi ambavyo anapambana kuhakikisha maendeleo yanawafikia Watanzania wote.

Mariam Ulega akisisitiza jambo kwenye mkutano huo(NA SHUSHU JOEL)

Akizungumza katika Baraza la jumiuya ya Umoja wa Wanawake Tanzania  (UWT) Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani alisema kuwa Rais Samia ni nguzo kubwa kwa wanawake kutokana kuwa mstali wa mbele katika kutatua CHANGAMOTO Ambazo zimekuwa zikiwasumbua wanawake kwa kipindi kirefu.

“ Wanawake nchini walikuwa na changamoto nyingi ambazo zilikuwa zikikwamisha mambo yao mengi kutokuendelea lakini tangu Rais Samia Suluhu Hassan ashike usukani vitu vingi vimekuwa vikienda kutokana na kupelekwa kwa fedha nyingi kwa jamii ili kumaliza changamoto hizo” Alisema Mariam Ulega

Aidha amewataka wanawake wote nchini kuendelea kuunga mkono juhudi kubwa ambazo zinafanywa na Rais wetu kipenzi Dkt Samia Suluhu Hassan kwani utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) umekuwa ukifanyika kila kukicha na wananchi wanajionea kile walichokuwa wakikihitaji kinafanikiwa kwa wakati.

Baadhi ya wanawake wa jumuiya hiyo wakimsikiliza Bi, Mariam Ulega kile anachowaelekeza katika mkutano huo.

Naye Mariam Masaninga ambaye ni diwani wa viti maalum amempongeza mjumbe huyo kwa ushauri mkubwa alioutoa kwa wanawake wa wilaya ya mkuranga.

Aidha amemtaka Mariam Ulega kuendelea kutoa ushauri kwani maneno yake yamekuwa yakijenga sana jumuiya na chama kwa ujumla.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments