“WAZAZI TUJIFUNGE MIKANDA KUOKOA TAIFA LA WATOTO WETU” ISLIM

Na Shushu Joel

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Temeke Khamis Islam akifuatilia jamabo kwa makini

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi kutokea Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Temeke Mkoa wa Dar es Salaam Khamis Islim amewakumbusha Wazazi umuhimu wa malezi bora na yenye msingi kwa watoto ili kuwasaidia watoto wetu kuweza kuwa na maadili mema kama waliyoyapata wao kipindi hicho.

Rai hiyo ameitoa alipokuwa akizungumza na viongozi mbalimbali wa Jumuiya hiyo katika moja ya vikao vyake anavyoendelea kuvifanya katika wilaya hiyo.

Aidha Mwenyekiti huyo alisema kuwa Wazazi wengi wamekuwa wakiiachia serikali sana malezi ya watoto wao bila wao kujihusisha na chochote kitu ambacho kinapelekea kukosekana kwa maadili mema ambayo sie enzi zetu tuliyapata.

“Vijana wetu wamekuwa na tabia za ajabu sana kile ambacho akikubaliki katika jamii” Alisema Islim

Pia alisema kuwa ni muhimu kutambua malezi bora yanaanza na wewe, Hivyo kama wazazi tunapaswa kusaidiana katika malezi sio mtoto wa jirani anapofanya kosa unamsubilia mzazi wake wakati na wewe ni mzazi na unapaswa kuonya kile kilichofanywa na motto huyo


Naye Ivonne Tibanywana ambaye ni mjumbe wa kamati ya utekelezaji jumuiya ya wazazi wilaya akiwakilisha vijana kutokea wazazi amempongeza Mwenyekiti huyo kwa kutambua kuporomoka kwa malezi mema kwa vijana wa kisasa hivyo yeye kama mwakilishi wa kundi hilo atahakikisha ujumbe huo unawafikia vijana kila kukicha.

Aidha amemuomba mwenyekiti huyo wa wazazi kuendelea kupaza sauti ili kuhakikisha jambo hilo la maadili kwa vijana linarudi kwenye nafasi yake.

MWISHIO

 

Post a Comment

0 Comments