Na Shushu Joel,Bagamoyo
MBUNGE wa viti maalum kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Pwani Subira Mgalu amesema kuwa vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto na wanawake vinazidi kuongezeka nchini na hivyo kupelekea wanawake walio wengi kudumaa kiuchumi
Mbunge wa viti maalu Mkoa wa Pwani Subira Mgalu akifafanua jambo mbele ya wanawake wa kata ya Fukayosi (NA SHUSHU JOEL)
Mgalu
alisema hayo hivi karibuni wakati alipokuwa akiongea na wanawake wa kata ya
Fukayosi iliyoko wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani kwenye uzinduzi wa mradi wa
maji safi na salama ulijengwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt
Samia Suluhu Hassan.
Alisema kuwa
takwimu za mwaka 2021 zinaonyesha kuwa Zaidi ya watoto asilimia 15% wamefanyiwa
ukatili hivyo hali hii inapelekea kudumaza uchumi wa wanawake kutokana na wengi
wao kujikita kupambania afya za watoto wao na kuacha kuendesha shughuli zao za
uchumi.
Aidha
aliongeza kuwa kutokana na kuongezeka kwa matukio hayo ya kikatili kuongezeka
nchini, Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dtk Samia Suluhu Hassan imeamua
kulivalia njuga jambo hili na kuamua kuja na mikakati ya uwezeshaji kiuchumi
makundi hayo kwa lengo la kuwa na biashara za kufanya.
Mbali na
hilo Mgalu amewataka wanawake kuendelea kuunda vikundi mbalimbali ambavyo
vitaweza kukopesheka kwa urahisi kwenye halmashauri zetu mbalimbali.
“Nitawaletea wataalamu mbalimbali kutoka benki ili waje wawapatie elimu juu ya uendeshaji wa biashara” Alisema Subira Mgalu
Kwa upande
wake Diwani wa kata hiyo Ally Ally amempongeza Mbunge wa viti maalum Subira
Mgalu kwa jinsi ambavyo amekuwa msaada kwa wanawake wa Mkoa wa Pwani katika
masuala mbalimbali na hasa ya upingaji ukatili na lile la kuwasaidia kukuza
uchumi wao kimakundi na binafsi.
Aidha
amemtaka aweze kuendelea na moyo huo wa kujitoa kwa jamii hivyo inaonyesha kuwa
ni jinsi gani Mgalu alivyo msaidizi sahihi kwa Rais wetu Dkt Samia Suluhu
Hassan.
Naye Bi,
Aisha Muhamed amempongeza Mbunge Subira Mgalu kwa jinsi ambavyo amekuwa
akiwapambania katika kupinga ukatili na kukuza uchumi wao,
MWISHO
0 Comments