Na Shushu Joel
![]() |
Mariam Ulega akiwakabidhi viongozi wa Shivyawata zawadi (NA SHUSHU JOE) |
MWENYEKITI
wa Jukwaa la Kuwezesha Wanawake Kiuchumi kutokea Mkoa wa Pwani Bi, Mariam Ulega
amekutana na watu wasiosikia ( Viziwi)
kupitia kwenye taasisi yao ya shivyawata na kufanikiwa kutoa misaada mbalimbali
kwa wahitaji hao.
Akizungumza
wakati alipokuwa akiwakabidhi mahitaji hayo Mariam Ulega alisema kuwa ameguswa
na watu hao wenye uhitaji na ndio maana amewasaidia vitu hivyo.
Aidha
alisema Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan
anatambua uwepo wa watu hao hivyo naye amekuwa kiungo kikubwa kwa wahitaji kama nyie ndio maana amekuwa
akitoa misaada mingi kwa wahitaji ili waweze kujikwamua kutoka sehemu moja
kwenda nyingine.
“Rais wetu Dkt Samia Suluhu Hassan ametoa fedha ili kuhakikisha walemavu wa aina zote wanakopesheka kupitia halmashauri wanazoishi kwa kuunda vikundi ama hata mmoja mmojahivyo niwaombe kuweza kuchangamkia fursa hizo ambazo zitawakwamua kiuchumi” Alisema Mariam Ulega Mwenyekiti wa Jukwaa la wanawake.
Picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiana zawadi
Mbali na
kuwakabidhi mahitaji hayo Bi, Mariam Ulega amewataka walemavu hao kutembea
kifua mbele kwani Rais Dkt Samia amekuwa ni nguzo kubwa kwa watanzania wote na ndio mana amekiwa
akisisitiza jinsia zote kuwajibika.
Kwa upande
wake Mwenyekiti wa idara ya wanawake na watoto shirikisho la vyama vya watu
wenye ulemavu Tanzania (shivyawata) Bi, Nasirya Ally amempongdza Mariam Ulega kwa jinsi amavyo
amekuwa msaada kwao na hasa kwenye utoaji wa misaada mbalimbali ambayo amekuwa
akiwapatia wao.
Aidha
amemtaka kuendelea na moyo huo huo na Mungu atamsaidia kwani Mungu anawapenda
watu wanawasaidia wenzao.
MWISHO
0 Comments