Na Shushu Joel
Mwakilishi wa Mjumbe wa kamati ya siasa Mkoa wa Pwani Alhaji Mansour Ndugu Mohamed Sheikh Mwenye tisheti Nyeusi akikabidhi futari kwa viongozi wa CCM Mkoa( NA SHUSHU JOEL)
MJUMBE wa kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani Ndugu Mussa Mansour amegawa futari kwa viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa ngazi za kata, wilaya na Mkoa.
Akizungumza
wakati wa zoezi hilo la ugawaji futari
hiyo mwakilishi wa Mjumbe huyo
ndugu Mohamed Sheikh alisema kuwa futari iligawia ni kuonyesha upendo kwa watu
wenzake kama vinavyosema vitabu vya dini.
Aliongeza
kuwa Alhaji Mansour amewataka wananchi kuendelea kuwa na umoja na upendo wa
dhati kwa Taifa letu ili kizazi kijacho kiweze kutambua thamani ya nchi yetu.
Aidha
Mwakilishi huyo wa Alhaji Mansour amewataka wazazi na walezi kuendelea kuungana
kwa pamoja ili kuweza kupinga vitendo vya ovyo vinavyofanywa na baadhi ya watu
kwa kuwalawiti watoto na hata kukemea vitendo vya ushoga ambavyo Rais wetu Mama
Samia Suluhu Hassan amekuwa akivikemea sana.
Pia amewataka wananchi wa Mkoa wa Pwani kuendelea kuwaombea viongozi wetu ambao wamekuwa ni chachu ya maendeleo kwa Tifa letu ili waweze kuendelea kuleta maendeleo kwa wananchi.
“Tuendelee
kuwa na moyo wa upendo na wa kujitoa kama ambao amekuwa akiufanya Alhaji
Mansour kwani ni mtu ambaye ni mwenye hofu ya Mungu” Alisema Mohamed
Naye Amina
Makona ambaye ni katibu wa vijana
(UVCCM) wilaya ya Kibaha amempongeza Alhaji Mansour kwa moyo wake wa upendo
aliounyesha kwa viongozi mbalimbali wa CCM.
Aidha
amewataka viongozi wengine kuiga mazuri ambayo yamekuwa yakifanywa na mjumbe
huyo wa kamati ya siasa Mkoa.
MWISHO
0 Comments