MJUMBE KAMATI YA SIASA PWANI NDUGU MANSOUR ASHIRIKI IBADA YA UMRA MAKKA

Na Shushu Joel

MJUMBE wa kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani Ndugu Mussa Mansour ameshiriki katika ibada ya Umra Makka.

Mussa Mansour mwenye kibegi akiwa katika sambamba na waumini mbalimbali katika ibada ya umra akipata Dua( na shushu joel)

Akizungumza kwa njia ya simu Mansour alisema kuwa ni vyema kila mmoja wetu akawa karibu na MOLA kwani dunia ni mapito hivyo ni vyema kutengeneza amana kubwa kwa muumba wetu.

Alisema kuwa matendo mema ni sadaka kubwa na pia tuendelee kumuomba  ALLAH aweze kuzikubali Dua zetu ili sisi wote kwa pamoja tuweze kuwa na mwisho mwema.

“Hakika hii Dunia ni mapito na ina mazuri mengi sana na kuna kila aina ya safari ambazo zitakupeleka katika kila pembe uitakayo lakini kona iliyo bora ni ile itakayokuweka karibu Zaidi na MOLA wako” Alisema Mansour

Aidha aliongeza kuwa ametumia nafasi hiyo kuwaombea watanzania wote ili nchi yetu iendelee kuwa na neema Zaidi.

 Pia alisema kuwa katika ibada hiyo amezidisha maomba kwa ajili ya Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan aweze kupata maisha marefu na yenye baraka tele.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments