Na Shushu Joel, Temeke
WILAYA ya Temeke iliyoko Jiji la Dar es Salaam imeanza mikakati ya maandalizi ya kushiriki mashindano ya Wazazi Cup yanayotarajia kuanza hivi karibuni ambayo yatafanyika katika uwanja wa uhuru maarufu shamba la Bibi.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Temeke Khamis Slim akifafanua jambo mbele ya makatibu kata(NA SHUSHU JOEL)
Akizungumza
kwenye kikao kazi cha maandalizi ya michuano hiyo Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Wazazi (CCM) Wilaya hiyo ya Temeke Khamis Slim alisema kuwa tumeamua kuanza
maandalizi ya michuano hiyo mapema kwa kusudi la kubeba ubingwa.
Alisema kuwa
wilaya ya Temeke ni wilaya pekee yenye viwanja vya mpira vya kisasa ikiwemo
uwanja wa Uhuru na kile cha Mkapa maarufu Lupaso hivyo kutokana na uwepo wa
viwanja hivyo ni lazima ubingwa uwe kwetu na hiki ndicho kilichopelekea kuanza
kwa maandalizi mapema.
“ Nimekutana
na makatibu wa wazazi wa kata zote za wilaya ya Temeke ili kuweza kuanzisha
mashindano madogo ndani ya kata zao ili waweze kuchagua vijana wataokao weza
kuunda timu mbili za jimbo ambazo zitakwenda kushindana na timu za wilaya
zingine za Mkoa wa Dar es Salaam” Alisema Slim
Aidha
Mwenyekiti huyo wa Wazazi amewataka vijana wote watakaopata nafasi ya
kuchaguliwa na kuunda timu za wilaya ya Temeke wahakikishae wanatumia nafasi
hii kuonyesha kipaji chao ili waweze kufika mbali kwani michezo ni ajira.
Alisema kuwa
wilaya ya Temeke ndio wilaya pekee hapa nchini inayomiliki viwanja viwili vya
viwanja vya mpira vya kisasa hivyo ubingwa ni laima uje temeke kutokana na
vipaji lukuki vilivyo jaa kwenye wilaya hiyo.
Naye katibu kata ya Mbagala Mtupa alisema kuwa kuanzishwa kwa Wazazi Cup kunakwenda kufungua milango kwa vijana wa wilaya yetu kuweza kujitangaza kupitia vipaji vyao hivyo wanatakiwa kupambana ili kuonekana kama ilivyokuwa kwa vijana wengine ndani nan je ya nchi ambao wametumia fursa za michozo kuonyesha vipajai vyao na hata kutimiza ndoto zao.
Hivyo
amesema kuwa jumuiya ya Wazazi imekuja na wazo zuri ambalo linakwenda
kuwasaidia vijana wa nchi hii pasipo na wasiwasi wowote ule.
Naye Kaimu
mratibu wa michezo wa mashindano hayo Bi,Ivonn Elias amehaidi kuwasaidia vijana
hao kwa lengo la kutimiza ndoto nzao za kucheza mpira wa miguu.
Aidha
amesisitiza juu ya nidhamu kwa wachezaji kwani nidhamu ndio kila kitu katika
michezo hivyo kama mtu hana nidhamu ni bora tu akaacha kucheza mpira
MWISHO
0 Comments