Na Shushu Joel,Mkuranga
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi (CCM) wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani Juma Mahege amesema kuwa Jumuiya hiyo ni chachu ya maendeleo na malezi bora kwa watoto hapa Nchini.

Mwenyekiti wa Wazazi wilaya ya Mkuranga Juma Mahege akisisitiza jambo kwa viongozi wa ccm.( NA SHUSHU JOEL)
Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo
alipokuwa akizungumza na wana Chama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Mgawa
.
Alisema kuwa
Jumuiya hii ni nguzo kubwa katika mambo
mengi hivyo kila kiongozi aliye ndani ya jumuiya yetu ni muhimu kuweza kujitafakali
kwa kina juu ya uwezo wake wa kuongoza na kusaidia jamii yetu katika Nyanja
mbalimbali.
Aidha
amewataka viongozi wa jumuiya hiyo kuendelea kuyasema yale mazuri yanayofanywa
na Rais wetu wa jamhuri ya Muungno wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwani
maendeleo anayoyafanya yamezidi kuwa msaada mkubwa kwa wananchi waTanzania.
“ Sasa hivi
kuna mashule, zahanati, vituo vya Afya , miundombinu bora ,umeme, maji na
mengine mengi ambayo Rais wetu amekuwa akiyafanya” Alisema Mahege’
Naye katibu wa ccm wa kata hiyo Miraji Msumi alisema Mwenyekiti wa wazazi wilaya ya Mkuranga ametuachia deni kubwa wana ccm hivyo tuna mwakikishia tutafanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha ccm inazidi kuwa juu kama ilivyo sasa.
Aidha
amewataka viongozi kuyafanyia kazi maneno yaliyosemwa na mwenyekiti wa Wazazi
ili kuweza kuongeza ufanisi wa utendaji kazi.
Pia katibu
huyo amempongeza mbunge wa Jimbo hilo ambaye pia ni Waziri wa Mifugo na
Uvuvi Abdallah Ulega kwa jinsi ambavyo
amekuwa msaada mkubwa katika ufanisi wa ufanikishaji wa maendeleo katika kata
hiyo kwani awali kata hiyo ilikuwa nyuma sana lakini sasa hivi tunaweza kusema
kuwa Ulega ni mfano wa kuigwa.
MWISHO

0 Comments