LAWRENCE TSINGAY ASHUSHA NEEMA KWA VIJANA WA BODABODA


 NA MWANDISHI WETU

Mjumbe wa kamati ya utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani  Ndugu Lawrence Peter Tsingay, amekabidhi seti moja ya jezi na mpira mmoja kwa vijana wa  bodaboda wa Mdaula kata ya Bwilingu 

Aidha alisema kuwa ni vyema vijana  kujiepusha na mambo yasiofaa na kushiriki kwenye michezo kwani michezo inaondoa mambo mengi ya kishawishi

 Pia aliongeza kuwa ni vyema  kuwaunga mkono viongozi waliotokana na Chama Cha Mapinduzi, diwani, mbunge na rais. "Shikeni michezo kwenye muda wenu wa ziada, itawasaidia kujiepusha na mambo yasiyofaa kwakuwa nyinyi bado vijana damu zenu zinachemka. 

Aidha aliongeza kuwa ni vizuri Tuwaunge mkono viongozi wanaotokana na CCM kuanzia diwani wetu, Mh mbunge Ridhiwani Kikwete  kwa uchapa kazi wake kama mnavuojionea miradi mikubwa kutokana na jitihada zake lakini pia amesisitiza tumuunge mkono Mh Rais, Dkt Samia Suluhu Hasani."

Kwa upande wake mmoja wa viongozi wa Boda boda Huseein Ally alisema kuwa mjumbe huyo ni mfano wa kuigwa kwa vijana kutokana na moyo wake wa kujitoa kwa vijana na jamii kwa ujumlahivyo amewataka wengine kuiga mfano huo.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments