UVCCM GEITA WATOA TAMKO ZITO

Na Shushu Joel, Bukombe

MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Geita Manjale Magambo wametoa tamko kuwa kwa Mwana chama  yeyote yule wa ccm  atakayechukua fomu ya kugombea nafasi ya Urais kupitia Chama hicho jumuiya ya vijana Mkoa huo utamshughulikia.

Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Geita Manjale Magambo akifafanua jambo kwenye baraza la vijna


Rai hiyo wameitoa kwenye kikao cha Baraza la vijana la Mkoa huo ambacho  kilifanyika wilayani Bukombe ambapo walikubaliana kuwa kwa kipindi kijacho anayetakiwa kuchukua famu ya nafasi ya kugombea Urais ni yule kipenzi cha Watanzania ambaye ni Dkt Samia Suluhu Hassan hivyo hakuna mwingine wa kuchukua famu ya nafasi hiyo.


Alisema kuwa kama Umoja wa Vijana wameamua kutangaza tamko hilo hili jamii ijue kuwa Rais wa Jamhuli ya Muungano waTanzania Dkt Samia Suluhu Hassan amewakosha watanzania kwa kuwapatia maendeleo makubwa na ambayo hayajawai kutokea katika nchi hii lakini kipindi hiki yamefanyika kwa wingi.


“Hivyo sie kama vijana tunasema ni Dkt Samia Suluhu Hassan ndiye tunakwenda nae 2025 kwani ameonyesha nia kubwa ya kuwatumukia watanzania” Alisema Manjale

Naye Nelvin Salabaga ambaye ni mjumbe wa kikao hicho amempongeza Mwenyeki wa Uvccm Mkoa kwa kufikisha dhamira yetu vijana wa Mkoa wa Geita.

MWISHO

 

Post a Comment

0 Comments