CCM BUKOMBE YAJA NA MIKAKATI KABAMBE.


Na ShushuJoel, Bukombe
                                                                   
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita kimanza mikakati kabambe ya kuhakikisha inavuna wana chama wapya ili kujihakikishia ushindi katika chaguzi zijazo kwa kusudi la kuendelea kushika dola na kuwaletea maendeleo wananchi wa Tanzania.

Picha ya pamoja ya viongozi wa CCM wilaya ya Bukombe mara baada ya kikao kazi( NA SHUSHU JOEL)


Akizungumza na kamati tendaji za jumuiya zote za chama katibu wa CCM Wilaya hiyo Ndugu Leonard Mwakalukwa alisema kuwa ni vyema kuongeza idadi kubwa ya uvunaji wanachama wa chama cha mapinduzi.

Alisema kuwa ni vyema kila kiongozi wa tawi na wa kata kuhakikisha anatemelea wananchi wa eneo lake na kuwaeleza mazuri yanayofanywa na viongozi wa CCM chini ya Mwenyekiti wa Taifa Dkt Samia Suluhu Hassan na hasa yale ya maendeleo kwa watanzania ambao walikuwa na kiu kuwa kuona miradi mikubwa ikifanyika.

 

“Chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Bukombe imetekeleza ilani ya uchaguzi kwa asilimia kubwa sana kwa wananchi hivyo tunajivunia kuwa na viongozi wenye kutekeleza ahadi zao kwa vitendo kwa jamii” Alisema Mwakalukwa

Aidha katibu huyo wa CCM amempongeza  kuwa jimbo la Bukombe ambaye pia ni Waziri wa Nishati na Naibu Waziri Mkuu Mhe. Dotto Biteko kwa jinsi ambavyo amekuwa mstali wa mbele katika ufanisi wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa jamii.

Naye Mwenyekiti wa UWT Wilaya hiyo Bi, Julieth Simon amemsifu katibu kwa kuzidi kuwa mbunufu juu ya uvunaji wa wanachama wapya katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mtaa na ukle uchaguzi mkuu hapa mwakani.

Aidha amewataka viongozi wa chama na jumuiya kuweza kuyafanyia kazi maono yanayoelezwa na viongozi wetu ambayo yamekuwa na malengo ya kujenga chama chetu.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments