DKT BITEKO CHANZO CHA MAFANIKIO YA CCM BUKOMBE

Na Shushu Joel, Bukombe

MWENYEKITI wa Chma Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Bukombe Mkoani Geita Ndugu Matondo Lutonja amempongeza Mbunge wa Jimbo hilo ambaye pia nia Waziri wa Nishati na Naibu Waziri Mkuu kwa jinsi ambavyo amekuwa mstali wa mbele katika mafanikio ya chama katika Nyanja mbalimbali za kimaendeleo ambazo awali ilikuwa ni ndoto lakini kipindi chake mambo yamezidi kuwa mbele.

Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Waziri wa Nishati na Naibu Waziri Mkuu Dkt Dotto Biteko akifafanua jambo mbele ya wajumbe ambao hawapo pichani.( NA SHUSHU JOEL)

Hayo amesema alipokuwa akizungumza na mabalozi wa wilaya hiyo katika ukumbi wa ccm wa wilaya.

Aliongeza kuwa Dkt Biteko amekuwa msaada mkubwa katika maendeleo ya chama na mpaka hapo tulipo sasa zimetrumika nguvu nyingi kutoka kwake .


Aidha Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa ni vyema kila kiongozi aliyepewa dhamani na chama cha mapinduzi kuhakikisha anawajibika kwa bidii na kuwa msaada mkubwa kwa kuwatumikia wananchi vile wanavyohitaji .


“Dkt Biteko amekuwa kiongozi wa pekee katika kukisaidia chama na hiki ndio chnazo cha kuzidi kuvuna wapinzani katika sehemu mbalimbali”Alisema Mwenyekiti Lutonja.


Kwa upande wake mmoja wa mabalozi mzee Ally  Juma alisema kuwa hakuna asiyeona kile kinachofanywa na Mbunge wetu katika Nyanja ya maendeleo wilayani kwetu hivyo uongozi wa Dkt Biteko mumekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wa Bukombe.

MWISHO

 

Post a Comment

0 Comments