"KAZI YA POLISI NI KAZI TAKATIFU" INSPECTOR OSWARD

Na Shushu Joel, Singida 


Askari wa Jeshi la Polisi Mkoani Singida  wametakiwa kutambua kuwa kazi ya Polisi ni kazi takatifu ambayo majukumu yake yanahusiana na makatazo na amri za Mungu.

Ispector Osward akifafanua jambo mbee ya wananchi waiojitokeza kwenye moja ya mikutano yake anayoifanya kwa jamii.


Kauli hiyo imetolewa na  Inspector wa Polisi kata  ya Ikanoda  Inspector  Osward alipofanya kikao na Wananchi mbalimbali wa kata hiyo


“Makatazo yaliyoandikwa kwenye vitabu vitakatifu yana mahusiano makubwa na kazi ya Polisi hasa katika amri za Mungu ambazo katika nyumba za ibada wanaziita dhambi huku kwetu ni uhalifu inatupasa kuzuia vitendo hivyo ili jamii iwe salama” Inspector Osward 


" Niwakumbushe jambo la muhimu wananchi wenzangu kuwa ni vyema  kuwa wamoja katika kutokomeza masuala ya ualifu ili kata yetu iwe takatifu kama yalivyo maandika" Osward 


Naye,Mwenyekiti wa kijiji cha Mjughuda  kata ya Ikhanoda Athumani Mohamed  aliwasisitiza wa i  kufanya kazi kwa bidii kwa kuzingatia wimbo wa maadili na kauli mbiu ya kazi iendelee hivyo ni vyema kumpa ushirikiano Inspector Osward ili kulifanya kazi ya polis kuwa nyepesi.


MWISHO

Post a Comment

0 Comments