MKAA WA STAMICO KUWEKA HISTORIA YA KUZUIA UKATAJI MITI.

Na Shushu Joel,Kisarawe

CHANGAMOTO kubwa ya ukataji wa miti kwa ajili ya uchomaji wa mkaa inakwenda kumalizika mara baada ya kumalizika kwa kiwanda cha utengenezaji wa nishati ya makaa ya mawe kukamilika katika wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani.

Kiongozi wa mbio za mwenge akipewa maelezo ya kiwanda cha makaa ya mawe na mkurugenzi wa Raslimali watu na utawala wa stamico( NA SHUSHU JOEL)


Akizungumza katika shughuli za ukaguzi wa kiwanda hicho ambapo Mwenge wa uhuru umekagua ujenzi huo, Mkurugenzi wa Raslimali watu na utawala  stamico Ndugu Deusdedith  Magala alisema kuwa kukamilika kwa kiwanda hicho ni suluhu la ukataji miti kwa ajili ya uchomaji mikaa.

“Kukamilika kwa kiwanda hiki kinakwenda kufungua ajira kwa watu mbalimbali wa wilaya ya kisarawe na wengine wengi” Alisema Mkurugenzi Raslimali watu na utawala wa STAMICO Magala

Aidha aliongeza kuwa ni vyema sasa watanzania kukipokea kiwanda hicho na kikubwa kununua na kutumia nishati ya makaa ya mawe kwani ni bei nafuu na yenye uwezo mkubwa kuliko matumizi ya mkaa.


Kwa upande wake kiongozi wa mbio za mwenye kitaifa Godfrey Mzava alisema kuwa ni jam,bo jema serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imefanya kwa ujenzi wa kiwanda cha makaa yam awe ambayo yanayokwenda kuwa suluhu ya utunzaji wa mazingira jambo ambalo limekuwa likipigiwa kelele sana.

Aidha Mzava amewataka stamico kuweza kuongeza nguvu ya ujenzi wa kiwanda hicho ili kiweze kuanza kazi mara moja.

Pia amewakumbusha stamico kuwa kiwanda hicho kinakwenda kuhakisi kauli mbiu yam bio za mwenge mwaka huu ambapo inasema kutunza mazingira na shiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa hivyo mazingira ni yetu lazima tuyatunze kwa nguvu kubwa .

MWISHO

Post a Comment

0 Comments