M/KITI WAZAZI BAGAMOYO AMUHAKIKISHIA USALAMA WA CHAMA KATIBU MKUU WAZAZI TAIFA

 Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Wilaya Bagamoyo Bw Aboubakary Mlawa  amemuhakikishia Katibu Mkuu wa wazazi Taifa Bw Ally Hapi kuwa Chama cha mapinduzi kipo salama  na kitaendelea kuwa salama.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Ndg Hapi akiteta jambo na Mwenyekiti wa Wazazi Wilaya ya Bagamoyo Mlawa( Na Shushu Joel)


Akitoa salamu za Chama na Jumuiya wakati wa kumkaribisha Katibu Mkuu hyo Mlawa alisema  Kamati ya siasa inaendelea kusimamia sSetikali na kuleta amani na ushirikiano wa wanachma kama kawaida   na hasa kipindi hiki ambacho Mwenyekiti wa Chama wilaya kutokuwepo kutokana na kuvuliwa Uongozi na Kamati kuu ya CCM  Taifa.


"Ndugu Katibu Mkuu pmoja na jahazi la uongozi kukumbwa na dhoruba  nna Nahodha kuishia njiani lakini manahodha wengine tupo na chombo kitaendelea na safari  "Alisema  Mlawa.


Naye Katibu Mkuu wa Jumuiya ya wazazi Taifa Ndugu Ally  Hapi aliwataka ushirikiano na miakikakati iwepo  kwa ajili ya chaguzi zilizo mbele za aerials ta Mitaa.

Akisema si muda  muafaka wa kujadili kimetokea nini na sababu gani,bali wanaccm ni wakati wao kuonyesha ushirikiano na kupanga mikakati ya kuhakikisha Chama kinashinda kwa kishibdo.

Post a Comment

0 Comments