WAVESLEEK WALETA AHUENU KWA WATANZANIA HASWA KWA WAPANGAJI WA NYUMBA

  NA Richard Mrusha

KAMPUNI ya Wavesleek kupitia Mtandao wao wa Seto waja na suluhisho Kwa wapangaji wa majumbani na hotelini kupitia Huduma ya kiganjani kwa bei nafuu ambapo pia inawapa fursa ya kujitengenezea kipato .

Mmiliki wa Kampuni ya Wavesleek Hamza Jabir akizungumza na waandishi Wahabari mara baada ya kuzindua  Mtandao wa "Seto" wenye lengo la kurahisisha upatikanaji wa Nyumba, sehemu za biashara Kwa wanaohitaji kupanga kupitia simu zao za Viganjani.

Akizungumza na waandishi Wahabari Mmiliki wa Kampuni ya Wavesleek Hamza Jabir amesema kutokana na kuwepo kwa changamoto  wanaopata watu wanaotafuta Makazi pamoja na sehemu za biashara Kampuni hiyo imetambulisha rasimi Huduma hiyo ya Mtandao mpya wa "Seto" ili kusaidia upatikanaji kwa haraka na bila usumbufu wowote.

Mtandao huu unalenga kurahisisha upatikanaji wa Nyumba sehemu za biashara   kupitia Mtandao wa Setto Kwa kupakua na kujisajiri na malipo  yake ni shilingi elfu 10 tu.

Hata hivyo ameeleza  kwamba mwanzo ilikua Ani usumbufu mkubwa Kwa kuwapatia Madalali pesa ya Kodi Kwa mwezi Mmoja hivyo basi kuwepo kwa Mtandao huo utaweza kuleta ahueni kwa wananchi."

AmesemaJabir  kuwa Kwa vijana ambao wamekosa Ajira Kwa kupitia Huduma hiyo ya Mtandao huo Seto wataweza kujipatia Ajira Kwa urahisi kama Madalali.

" Nawaomba vijana wachangamkie fursa hiyo ya udalali kupitia Mtandao wa Setto Kwa kusambaza picha za  Nyumba ambazo zinapangishwa au kuuzwa, Kwa kufanya hivyo wataweza kupata shilingi elfu 6 kama malipo yao."a

Post a Comment

0 Comments