MARIAM ULEGA TEGEMEO JIPYA LA WANAWAKE PWANI.

Na Shushu Joel, Rufiji

WANAWAKE wa Mkoa wa Pwani wameambiana kutembea kifua mbele kwa kipindi hiki kutokana na kile walichokifanya katika uchanguzi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mara baada ya kumpigia kura za kishindo na kumchagua Mariam Ulega kuwa Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Wanawake Tanzania  (Mbaraza) kutokana na kile ambacho ameanza kuwaonyeshea wanawake wa Mkoa huo.

Mariam Ulega akiwa katika moja ya heka heka heka zake(NA SHUSHU JOEL)

Rai hiyo imetolewa na baadhi ya wanawake wa Mkoa huo kwa  kusema kuwa sababu ya mambo ambayo yamekuwa yakifanywa na kiongozi huyo ya kuwasaidia wanawake wa Mkoa huo ili waweze kuondokana na baadhi ya changamoto mbalimbali ambazo zilikuwa zikiwakabili wanawake wa Pwani.

Fatma Mapanga ni mkazi wa wilaya ya Bagamoyo alisema kuwa Mbaraza wetu Mariam Ulega ni kiongozi mwenye uchungu mkubwa na jumuiya yetu ndio maana amekuwa akikutana na wanawake wa Mkoa wa Pwani mara kwa mara na kuwapatia mafunzo ya kila namna ili  mradi tu aweze  kuwainua kiuchumi wanawake wa maeneo mbalimbali katika Mkoa wa Pwani.

Aidha alisema kuwa wanawake tunatakiwa kuiga yale yanayofanywa na Maria Ulega kutokana na kile ambacho amekuwa akikihakikisha kinawafanikishia wanawake katika kukuza uchumi wao wa kila siku ili waweze kuondokana ana matatizo ya kuwategemea waume zao.

“Kwa kweli kipindi hiki tumefanikiwa kupata kiongozi ambaye tuna matumaini naye makubwa kuwa anaweza kutuvusha na kufika mbali sana kutokana na kiu yake ya kuwaona wanawake wenzake wana kuwa na uchumi wa kujitegemea na kuondokana na utegemezi kutoka kwa wanaume” Alisema Bi. Fatma

 

Kwa upande wake Mariyam Masaninga amempongeza Mbaraza Mariam Ulega kwa jinsi ambavyo amekuwa akijitoa maisha yake ili kuwasaidia wanawake wa Pwani waweze kuinuka na kuachana na tabia ya kuwa tegemezi kwa wanaume.

 

Aidha aliongeza kuwa uimara wa Mjumbe huyo wa Mkutano Mkuu wa UWT ni kutokana na kiu kubwa aliyonayo ya kuhitaji wanawake wote wasonge mbele kiuchumi .

Akizungumza kwa njia ya simu Mjumbe huyo mara baada ya kupigiwa simu alisema lengo ni kuhakikisha wanawake Mkoa wa Pwani wanakuwa kiuchumi kwa lengo la wao.

Aidha amewapongeza wanawake kwa ushirikiano waliompatia tangu apate nafasi hiyo ya ujumbe kwani peke yake ni sawa na bure hivyo kwa umoja huo tunaweza kufika mbali katika kumsaidia Rais Dkt Samia Suluhu Hassan

MWISHO

Post a Comment

0 Comments