MENEJIMENTI YA TAWA YATAKIWA KUFANYA KAZI KWA USHIRIKIANO

Na Shushu Joel

 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb)ameitaka

menejimenti Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA)

ifanye kazi kwa ushirikiano ili kuiwezesha taasisi hiyo kutimiza malengo

yaliyowekwa.

 Mhe. Mary Masanja ametoa kauli hiyo leo jijini Mwanza mara baada ya

kuitembelea menejimenti ya TAWA inayoendelea na mafunzo ya uongozi

katika Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Pasiansi.


Amewaeleza kuwa utendaji kazi wenye kuzingatia ushirikiano na Upendo ni

nguzo muhimu itakayowawezesha kurekebishana na kukosoana kiutendaji

kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa.


Aidha, amesisitiza kuwa ni vyema menejimenti hiyo ikajiwekea utaratibu wa

kujadili changamoto mbalimbali pamoja ili iweze kufika mbali kiutendaji.

"Mwenzako anapokutana na changamoto yoyote ichukulie kama ni yako.

Tunahitaji tufanikiwe kwa kutatua changamoto zinazotukabili kwa pamoja "

amesisitiza Mhe. Masanja.


Mafunzo hayo yenye lengo la kuwajengea uwezo viongozi  katika usimamizi

wa masuala mbalimbali yakiwemo ya rasilimali watu, fedha na taratibu za

manunuzi yametolewa kwa Manaibu Kamishna, Makamanda wa Kanda,

Makamishna Wasaidizi Wandamizi na Makamishna Wasaidizi.

Post a Comment

0 Comments