NAIBU WAZIRI MASANJA AGAWA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 14 NA MITUNGI YA GESI 100 MAGU

NA SHUSHU JOEL

 Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza, ambaye pia ni Naibu Waziri wa

Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja akiwa ameambatana na Umoja wa

Wanawake wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Magu amegawa vifaa tiba

vyenye thamani ya shilingi milioni 14 kwa Hospitali ya Wilaya ya Magu

pamoja na mitungi ya gesi 100 kwa wanawake wajawazito.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mery Masanja akipokea pongezi kutoka kwa Mganga Mkuu wav Magu mara baada ya kukabidhi vifaa 

Akizungumza leo katika hafla ya ugawaji wa vifaa hivyo vyenye thamani ya

shilingi 14,575,000 na mitungi ya gesi 100 kwenye Hospitali ya Magu, Mhe.

Masanja amesema vifaa hivyo vimetokana na mchango wake binafsi pamoja

na mchango wa Doris Mollel Foundation.


Amefafanua kuwa vifaa tiba hivyo vitasaidia kuokoa maisha ya watoto

waliozaliwa njiti na pia mitungi ya gesi itasaidia wanawake wajawazito

kupunguza shughuli nzito za kutafuta nishati mbadala.


Mhe. Masanja amewaasa wanawake wajawazito kuhudhuria kliniki mara kwa

mara ili kujua maendeleo ya mtoto anapokuwa tumboni.


Aidha, Mhe. Masanja amewataka wanawake wa Umoja wa Wanawake

Tanzania (UWT) kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada anazozifanya za

kuwaletea maendeleo wananchi wa Tanzania.


Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Magu Dkt.Maria Kapinga

amesema vifaa hivyo vilivyotolewa na Naibu Waziri Masanja vitasaidia

kunusuru maisha ya watoto wanaozaliwa kabla ya muda ( njiti).

Post a Comment

0 Comments