JUKWAA LA MAENDELEO YA UTAMADUNI KUSHIRIKIANA KUKUZA UTAMADUNI NCHINI

 Na Eleuteri Mangi-WUSM,Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu amekutana na

kufanya mazungumzo na Naibu Balozi wa Uswisi hapa nchini ambaye pia ni Mkuu wa

Mkuu wa Kitengo cha Ushirikiano wa Kimataifa Bw. Leo Näscher kuhusu ushirikiano

katika eneo la Utamaduni na Sanaa baina ya nchi hizo mbili.


Kikao hicho kimefanyika Machi 9, 2023 katika ofisi za Wizara hiyo yenye Makao yake

Makuu katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.


Katibu Mkuu Bw. Yakubu ameeleza azma ya Serikali katika kusimamia sekta za

Utamaduni, Sanaa na Michezo ambazo zinatoa ajira kwa vijana wengi na zina mchango

mkubwa katika ukuaji wa uchumi nchini na namna watakavyoshirikiana katika

kubadilishana utaalam na uzoefu katika sekta hizo.


Naye Bw. Leo Näscher Naibu Balozi wa Uswisi hapa nchini ambaye pia ni Mkuu wa

Kitengo cha Ushirikiano wa Kimataifa amesema wana Jukwaa la Maendeleo ya Sekta

ya Utamaduni (DGP) ambalo linaundwa na Balozi mbalimbali ambapo kwa sasa

linaongozwa na Wenyeviti ambao ni Uholanzi na Uswisi wataendelea kushirikiana na

Wizara hiyo na watakuwa kiunganishi na wadau mbalimbali wa sekta za Utamaduni na

Sanaa wakisaidia katika nyanja za utaalam na ushauri.

Post a Comment

0 Comments